Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 19 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 162 2017-05-08

Name

Angelina Adam Malembeka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza:-
Kuna vijana zaidi ya 300 Mkoa wa Kaskazini Unguja ambao wanajihusisha na kazi mbalimbali za kujitolea kama vile usafi, upandaji miti, kilimo cha mboga mboga na matunda na wapo tayari kijiunga na Jeshi la Ulinzi kama wakifikiriwa:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuwachukua vijana hao kujiunga na Jeshi hasa ikizingatiwa kuwa wana maadili mema na wameweza kujitolea?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Angelina Adam Malembeka, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, utaratibu wa sasa wa wananchi wa Tanzania kuajiriwa katika Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania unataka waombaji kuwa wamepitia Jeshi la Kujenga Taifa. Jeshi la Kujenga Taifa hutoa nafasi kwa kila mkoa. Vijana wanaopenda kujiunga na Jeshi hujadiliwa na kupitishwa na Kamati za Ulinzi na Usalama ngazi ya wilaya na mkoa husika. Kwa upande wa Zanzibar nafasi hizo hutolewa kupitia Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na idara maalum za SMZ. Ofisi hiyo ndiyo yenye wajibu wa kupeleka mgao huo katika mikoa husika.
Mheshimiwa Spika, kuhusu vijana zaidi ya 300 wa Mkoa wa Kaskazini Unguja ambao wanajihusisha na kazi mbalimbali za kujitolea na ambao wako tayari kujiunga na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania, vijana hao wanashauriwa kuomba kujiunga na Jeshi la Kujenga Taifa mara nafasi zitakapotangazwa. Endapo watakuwa na sifa za kuajiriwa na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania naamini watapewa fursa hiyo kwa kadri ya nafasi zitakavyopatikana.