Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 32 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 258 2017-05-23

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA (K.n.y. MHE. RIDHIWANI J. KIKWETE) aliuliza:-
Hivi karibuni kumetokea mapigano baina ya wakulima na wafugaji ambayo yamesababisha baadhi ya Watanzania kupoteza maisha na wengine kupata ulemavu wa maisha:-
Je, Serikali imejipangaje kupambana na janga hilo?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ridhiwani Jakaya Kikwete, Mbunge wa Chalinze, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kumekuwa na migogoro kati ya wakulima na wafugaji katika maeneo kadhaa ndani ya nchi yetu ambayo yamesababisha Watanzania kupoteza maisha na wengine kupata ulemavu wa kudumu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kukabiliana na hali hiyo Serikali kupitia Jeshi la Polisi inaendelea kushauriana na Mamlaka zinasosimamia matumizi bora ya ardhi, kutenga maeneo yatakayotumiwa na wakulima na wafugaji ili kuepusha migogoro na kutoa elimu kwa wakulima na wafugaji juu ya mazingira bora ya matumizi ya ardhi. Aidha, Jeshi la Polisi hufanya doria na misako na kukamata wale wanaovunja Sheria punde panapokuwepo na mwingiliano wa matumizi bora ya ardhi katika maeneo yanayosababisha migogoro.