Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 33 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 265 2017-05-24

Name

Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA aliuliza:-
Mwaka 2012/2013 Serikali ilichukua ardhi ya wananchi wa Mtwara Mjini eneo la Mji Mwema na Tangira. Aidha, Serikali imewazuia wananchi hao kufanya shughuli za maendeleo katika maeneo hayo. Serikali iliahidi kuwalipa wananchi hao fidia lakini hadi sasa fidia hiyo haijalipwa.
Je, ni lini Serikali italipa fidia kwa wananchi wao?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Maaftaha Abdallah Nachuma, Mbunge wa Mtwara Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, fidia stahiki itaanza kulipwa kwa wananchi 2,020 kuanzia mwezi Juni, 2017 hadi robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2017/2018. Taasisi ya UTT - PID kwa kushirikiana na Halmashauri inatarajia kutumia shilingi 7,523,000,000 kwa ajili ya malipo ya fidia kabla ya kuanza kwa kazi ya upimaji wa viwanja. Ofisi ya Rais - TAMISEMI ilitoa kibali cha kuendelea na utekelezaji wa mradi kupitia barua yenye Kumb. Na. GB. 203/234/01/117 ya tarehe 02/09/2016.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, ulipaji wa fidia haukuanza mapema kutokana na kampuni husika ya UTT -PID kutokuwa na Bodi. Bodi imeshaundwa na makubaliano ya pamoja yamefanyika katika kikao cha tarehe 02/05/2017 baina ya Mheshimiwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, UTT – PID na Halmashauri.