Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 2 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 18 2016-04-20

Name

Tauhida Cassian Gallos Nyimbo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAIDA MOHAMED BAKAR (K.n.y. MHE. TAUHIDA CASSIAN GALLOS NYIMBO) aliuliza:-
Je, Serikali ina mkakati gani wa kunusuru mauaji ya vikongwe nchini?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Tauhida Cassian Gallos, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Jeshi la Polisi imeweka mikakati mbalimbali ya kunusuru mauaji ya vikongwe nchini ikiwa ni pamoja na:-
(i) Kufanya operesheni na misako ya mara kwa mara kubaini waganga wa jadi wanaojihusisha na upigaji ramli chonganishi na wasiofuata sheria;
(ii) Kutoa elimu kupitia Polisi Jamii, wadau mbalimbali wa ulinzi na usalama, madhehebu ya dini na mashirika na taasisi binafsi, lengo likiwa ni kuwaelimisha wananchi madhara ya kujichukulia sheria mkononi; na
(iii) Kuanzishwa kwa vikosi kazi ili kuweza kufuatilia na kutafuta taarifa mbalimbali za watuhumiwa wanaotenda matukio hayo maarufu kama wakata mapanga, kabla na baada ya kufanyika kwa tukio.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nitumie fursa hii kwenye Bunge lako Tukufu kutoa rai kwa wananchi kuacha vitendo vya kujichukulia sheria mkononi vinavyosababisha mauaji kwa nchi yetu inaendeshwa kwa mujibu wa sheria.