Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 26 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 215 2017-05-16

Name

Ester Michael Mmasi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTER M. MMASI aliuliza:-
Kupitia fursa ya ujenzi wa bomba la mafuta Mkoani Tanga, ni dhahiri kwamba vijana takribani 15,000 watapata ajira kwenye mradi kwa upande wa Tanzania:-
(a) Je, Serikali imejipangaje kuona kuwa vijana wa Kitanzania wanapata ajira katika soko la Tanzania kupitia fursa hii ya uwekezaji?
(b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuingiza mtaala wa mafuta na gesi katika mitaala ya VETA ili kuwajengea uwezo, maarifa na ujuzi vijana wa Kitanzania katika sekta hiyo muhimu?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ester Michael Mmasi, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi wa ujenzi wa bomba la kusafirisha mafuta ghafi kutoka Hoima (Uganda) hadi Bandari ya Tanga (Tanzania) uko katika hatua ya majadiliano ya jinsi mradi huo utakavyotekelezwa. Katika majadiliano hayo, suala la ajira kwa Watanzania litazingatiwa ili Watanzania wanufaike na ajira kupitia ujenzi na uendelezaji wa mradi huo. Mradi unatarajiwa kutoa ajira 10,000 wakati wa ujenzi na ajira kwa watu 1,000 wakati wa uendeshaji.
(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2012 na 2013 Wizara ya Nishati na Madini kwa kushirikiana na Kampuni ya Petrobras ya Brazili, iliendesha mafunzo maalum ya ufundi wa plumbing, uchomeaji, upakaji rangi pamoja na mambo mengine katika Chuo cha VETA huko Mtwara na Lindi. Mafunzo hayo yalilenga kuwaongezea weledi wanafunzi wapatao 350 wa VETA ambao wamepatiwa vyeti vya kimataifa na wanaweza kuajiriwa ndani ya nchi na nje ya nchi. Gharama za mafunzo yote ni Dola za Marekani milioni nne.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa kushirikiana na Serikali ya Norway, chini ya Mradi wa Mafuta kwa Maendeleo (Oil for Development) imekamilisha taratibu za kuingiza mtaala wa mafuta na gesi katika vyuo vya VETA hapa nchini. Mtaala huu utaanza kutumika katika baadhi ya vyuo vya VETA hapa nchini mwaka 2018. Utekelezaji wa mpango huu utagharimu Dola za Marekani milioni 20.