Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 28 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 229 2017-05-18

Name

Mwantakaje Haji Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Bububu

Primary Question

MHE. MWANTAKAJE HAJI JUMA aliuliza:-
Kumekuwa na wimbi la mabweni na hata shule kuungua moto, hususan Tanzania Bara. Je, Serikali ina mpango gani wa kudhibiti hali hiyo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwantakaje Haji Juma, Mbunge wa Bububu, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kulikuwa na wimbi la shule kuungua moto na mwaka 2016 pekee kuanzia mwezi Januari hadi Disemba nchi ilikuwa na janga kubwa la kuunguliwa na shule za sekondari 29, zikiwemo mbili zisizo za Serikali na shule za msingi mbili ikiwemo moja isiyo ya Serikali.
Matukio hayo yalitokea mfululizo na hata shule nyingine kukumbwa na tatizo hilo zaidi ya mara moja. Mbaya zaidi, katika mwezi wa Agosti, 2016 kasi ya matukio ya shule kuungua moto iliongezeka ambapo kati ya tarehe Mosi hadi 12 Agosti, 2016 jumla ya shule za sekondari za Serikali tano ziliungua. Tumeshukuru Mungu mwaka 2017 matukio haya ya moto hayajatokea tena.
Mheshimiwa Naibu Spika, hadi sasa hakuna uhakika wa chanzo halisi cha matukio haya moto yanayojitokeza. Hata hivyo, inadhaniwa kuwa chanzo cha moto hususan katika shule kongwe ni hitilafu ya umeme iliyotokana na uchakavu wa miundombinu na hujuma kutoka kwa watu na vikundi visivyo na nia njema.
Mheshimiwa Naibu Spika, majanga ya moto katika shule zetu yanaweza kudhibitiwa ikiwa wote kwa pamoja tutashirikiana kutambua na kudhibiti viashiria na vyanzo ambavyo huleta majanga hayo. Serikali imetoa maelekezo kwa Mikoa, Halmashauri na wadau wengine wa elimu ili kudhibiti majanga ya moto mashuleni ikiwa ni pamoja na uundwaji wa Kamati za kukabiliana na majanga katika ngazi ya Halmashauri na katika ngazi za shule husika kwa kushirikisha wadau muhimu wa elimu katika ngazi mbalimbali.