Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 23 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 195 2017-05-12

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza:-
Wananchi wengi Sumbawanga hawana hati miliki; aidha, kumekuwa na changamoto nyingi katika kupata hati hiyo hali inayowafanya wananchi kukata tamaa.-
Je, ni gharama kiasi gani zinazohitajika ili kupata hati miliki?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Aida Joseph Khenani, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kawaida hati miliki za ardhi hutolewa kwa utaratibu wa mwombaji kuchangia gharamaza upatikanaji wa hati husika. Utaratibu huu umetokana na matakwa ya Sera ya Taifa ya Ardhi ya mwaka 95 ambayo inaelekeza kuwa ardhi ina thamani.
Mheshimiwa Naibu Spika, gharama za kupata hati miliki hutofautiana kutokana na thamani ya ardhi katika eneo linaloombewa hati, ukubwa wa eneo na matumizi yanayokusudiwa katika eneo husika. Kwa mantiki hiyo, gharama za kupata hati miliki hutofautiana kwa kuzingatia vigezo hivyo. Gharama zinazotakiwa kulipwa wakati wa umilikishaji ardhi ni kama ifuatavyo:-
Ada ya upimaji;
(ii) Ada ya uandaaji wa hati ambayo ni shilingi 50,000 ni fixed;
(iii) Ada ya usajili wa hati;
(iv) Ushuru wa stempu;
(v) Gharama za upatikanaji ardhi;
(vi) Ada ya mbele (premium) ambayo ni asilimia 7.5 ya thamani ya ardhi; na
(vii) Ada ya ramani ndogo (Deed Plan) ambayo ni shilingi 20,000 nayo ni fixed.
Mheshimiwa Naibu Spika, ada ya upimaji, usajili wa hati, ushuru wa stempu na gharama za upatikanaji ardhi hutegemea ukubwa na thamani ya ardhi katika eneo husika.
Mheshimiwa Naibu Spika, ili kuwa na uwiano wa gharama za umilikishaji wa ardhi nchini, Wizara imeandaa na kusambaza mwongozo wa ukadiriaji wa bei za viwanja kwa Halmashauri zote nchini. Mamlaka za Serikali za Mitaa kote nchini hazina budi kuzingatia mwongozo wa bei elekezi za viwanja uliotolewa ili kuwawezesha wananchi kupata hati miliki kwa gharama nafuu zaidi.