Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 40 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 322 2017-06-02

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Primary Question

MHE. OMARY T. MGUMBA aliuliza:-
Kuna vyanzo vingine mbadala ya maji katika Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki kama vile Mto Mbezi, Mto Ruvu na chanzo cha maji katika Kijiji cha Bamba Kiloka.
Je, Serikali ina mpango gani wa muda mfupi, kati na muda mrefu wa kutatua changamoto ya maji safi na salama katika vijiji vya Mkuyuni, Madam, Luholole, Kibuko, Mwalazi, Kibuko na Mfumbwe katika kupanua na kuongeza uwezo wa tanki la Mto Mbezi ili liweze kukidhi mahitaji ya sasa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Omary Tebweta Mgumba, Mbunge wa Morogoro Kusini Mashariki kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na utekelezaji wa miradi ya maji katika vijiji vya Fulwe unaogharimu shilingi bilioni 2.2; Gwata unaogharimu shilingi milioni 440.6; Chanyumbu unaogharimu shilingi milioni 785.7; Mkulazi unaogharimu shilingi milioni 216.7; Kibwaya unaogharimu shilingi milioni 627.2 na Kiziwa unaogharimu shilingi milioni 785.8. Aidha, halmashauri imepanga kutumia shilingi milioni 368.5 kwa ajili kufanya ukarabati na upanuzi wa miundombinu ya mradi wa maji katika kijiji cha Mkuyuni na Kivuma ambao unatumia chanzo cha maji cha Mto Mbezi.
Mheshimiwa Spika, katika mpango wa muda wa kati, Halmashauri imetenga shilingi milioni 150 kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa miradi ya maji ya mtiririko (gravity water schemes) ambao utahudumia vijiji vya Mwalazi, Luholole, Kibuko na Madam, Lubungo na Maseyu.
Mheshimiwa Spika, mpango wa maji wa muda mrefu utahusisha ujenzi wa miradi ya maji katika vijiji 19 vikiwemo vijiji kumi vya Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki. Miradi hiyo itagharamu shilingi bilioni 8.62 kuanzia mwaka 2017 mpaka 2021.