Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 8 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 17 2017-09-06

Name

Stephen Hillary Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. STEPHEN H. NGONYANI aliuliza:-
Serikali iliahidi kutoa shilingi milioni 60 kwa ajili ya mradi wa maji wa Sakare ulioko Tarafa ya Bungu na mpaka sasa imetoa shilingi milioni 20 tu; Je, ni lini fedha iliyobaki itatolewa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stephen Hillary Ngonyani, Mbunge wa Korogwe Vijijini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, mradi wa maji wa Sakare unahudumia jumla ya vijiji saba kutoka kwenye Tarafa ya Bungu vyenye wakazi wapatao 18,460. Ili kutekeleza ahadi iliyotolewa katika mwaka wa fedha 2017/2018, Serikali imeidhinisha shilingi milioni 81.5 kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa Sakare. Azma ya Serikali ni kuhakikisha mradi huo unakamilika kwa wakati ili wananchi wa vijiji saba katika Tarafa ya Bungu waweze kupata maji safi na salama.