Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 8 Sitting 3 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 31 2017-09-07

Name

Eng. James Fransis Mbatia

Sex

Male

Party

NCCR-Mageuzi

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. JOSEPH R. SELASINI (K.n.y. MHE. JAMES F. MBATIA) aliuliza:-
LEKIDIA imeweza kushirikiana na wananchi wa Kata ya Kirua Vunjo Mashariki na kufanikiwa kukarabati barabara za kata hiyo zenye urefu wa kilometa 17 kwa gharama ya shilingi milioni nane, lengo kuu ni ujenzi wa barabara inayoanzia Uchira hadi Kolaria yenye urefu wa takribani kilometa 12 kwa kiwango cha lami; na LEKIDIA wamefanikiwa kufanya harambee na kupata shilingi milioni 130 ambapo shilingi milioni 60 zimetumika kununua mapipa 300 ya lami na kubakiwa na shilingi milioni 70.
Je, Serikali itashirikianaje na LEKIDIA kutekeleza mradi huo kwa ajili ya maendeleo endelevu ya wananchi wa Kata ya Kirua Vunjo Mashariki?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa James Francis Mbatia, Mbunge wa Vunjo, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Uchira -Kisomachi - Kolaria yenye urefu wa kilometa 12 ilijengwa kwa kiwango cha changarawe kwa gharama ya shilingi milioni 300 kutoka katika Mfuko wa Barabara katika mwaka wa fedha 2013/2014. Barabara hiyo imeendelea kufanyiwa matengenezo ambapo katika mwaka wa fedha 2016/2017 zilitumika shilingi milioni 74.2 ili kuifanya ipitike wakati wote. Katika mwaka wa fedha 2017/2018, Serikali imepanga kutumia shilingi milioni 31 kwa ajili ya matengenezo ya kawaida kilometa nane na matengenezo ya sehemu korofi kilometa mbili.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunapongeza juhudi kubwa inayofanywa na LEKIDIA. Serikali kupitia Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini (TARURA) itafanya tathmini ya barabara zote nchini pamoja na barabara ya Uchira hadi Kolaria ili kuona namna bora ya kuziboresha barabara hizo kwa kiwango kinachohitajika.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kushirikiana na wananchi na wadau wengine wa barabara ili kuhakikisha barabara hiyo inafanyiwa matengenezo kurahisisha usafiri na usafirishaji.