Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 8 Sitting 7 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 92 2017-09-13

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itatengeneza miundombinu ya maji katika Hifadhi ya Mkomazi ili kuzuia wanyamapori kuzurura kwenye makazi ya wananchi wakitafuta maji na kuharibu mazao yao?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Naghenjwa Livingstone Kaboyoka, Mbunge wa Same Mashariki, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi inapatikana katika nyanda kame na hivyo kukabiliwa na uhaba wa maji kwa ajili ya matumizi ya wanyamapori. Wizara imefanya juhudi za kuchimba mabwawa kwa ajili ya kuhifadhi maji ambapo hadi sasa kuna jumla ya mabwawa tisa ambayo ni Mabata, Kuranze, Zange, Ndindira, Nobanda, Ngurunga, Mbula, Kavateta na Maore. Hata hivyo, kutokana na mabadiliko ya tabianchi ni mabwawa matatu tu yanahifadhi maji mwaka mzima.
Mheshimiwa Spika, kutokana na changamoto hiyo ya upungufu wa maji, Serikali inaendelea kuchimba mabwawa sita ili kukidhi mahitaji ambapo bwawa moja lilikamilika katika mwaka wa fedha wa 2016/2017 na mengine matano yatachimbwa katika mwaka huu wa fedha 2017/2018.
Aidha, katika mwaka 2017/2018 kisima kirefu kimoja kitachimbwa kwa ajili ya kusukuma maji na kujaza mabwawa yanayokauka ili kukidhi mahitaji ya maji wakati wa kiangazi kikali na wakati huo huo doria za kudhibiti wanyamapori wasitoke nje ya hifadhi zinaendelea kuimarishwa.