Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 5 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 42 2016-04-25

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER L. MIDIMU aliuliza:-
Wilaya ya Itilima ni moja kati ya Wilaya mpya zilizoanzishwa hivi karibuni ili kurahisisha utoaji wa huduma kwa wananchi:-
Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kuwezesha kujenga ofisi na nyumba za watumishi katika Makao Makuu ya Wilaya ya Itilima eneo la Itilima?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORAalijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Lukago Midimu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, mpango wa ujenzi wa nyumba za watumishi na viongozi katika Wilaya mpya ya Itilima umeshaanza na uko katika hatua ya ujenzi wa nguzo za jamvi. Fedha zilizopokelewa kwa kazi hiyo ni shilingi milioni 100 kati ya shilingi 500 zilizotengwa mwaka 2014/2015. Katika bajeti ya mwaka 2016/2017 zimetengwa tena shilingi milioni 500 ili kuendelea na ujenzi wa nyumba na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya.
Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Itilima imesaini Mkataba na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kwa ajili ya ujenzi wa nyumba saba za watumishi kwa gharama ya shilingi milioni 450 na fedha hizo zipo. Kati ya fedha hizo, shilingi milioni 47 zimetumika kuwalipia fidia wananchi waliohamishwa kupisha ujenzi huo. Vilevile katika bajeti ya mwaka 2016/2017 zimetengwa shilingi milioni 500 ili kuendelea na ujenzi wa nyumba na ofisi ya Halmashauri.