Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 8 Sitting 8 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 103 2017-09-14

Name

Twahir Awesu Mohammed

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mkoani

Primary Question

MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN (K.n.y. MHE. TWAHIR AWESU MOHAMMED) aliuliza:-
Tanzania ni nchi yenye amani kubwa katika nchi za Maziwa Makuu.
• Je, Serikali imejipanga vipi kuimarisha amani katika nchi yetu?
• Je, mipaka yetu na nchi zenye mizozo na wakimbizi imeimarishwa kiasi gani kiulinzi?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA aliuliza:-
Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Twahir Awesu Mohammed, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Spika, kimsingi suala la kuimarisha usalama na amani ya nchi yetu ni jukumu la kila Mtanzania. Hata hivyo, Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania ambalo ndilo lenye jukumu la kulinda mipaka yetu ya Kimataifa na kuimarisha amani nchini limekuwa likishirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama pamoja na wadau wengine kuhakikisha kuwa hakuna adui wa ndani au wa nje anayeweza kuhatarisha au kuvuruga amani ya nchi yetu.
(b) Mheshimiwa Spika, Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania limejipanga kikamilifu katika kuhakikisha kuwa mipaka ya nchi yetu inalindwa muda wote dhidi ya adui yeyote atakayejitokeza kuivamia.
Aidha, Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania kwa kushirikiana na vyombo vingine vya usalama limeimarisha ulinzi katika maeneo ya mipaka yenye wakimbizi kwa kuweka viteule na vifaa vya kutosha. Hatua hii imesaidia kuzuia na kukabiliana na vitendo vyote vya kihalifu vinavyoweza kusababishwa na wakimbizi katika mipaka na katika makambi waliyopangiwa.