Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 34 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 274 2017-05-25

Name

Jaku Hashim Ayoub

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. JAKU HASHIM AYOUB aliuliza:-
Kuna mjenzi aliyejenga Vituo vya Polisi kupitia Kampuni iitwayo Al Batna Building Co. Ltd. Vituo alivyojenga ni Kituo cha Polisi Mkokotoni - Unguja na Kituo cha Polisi cha Madungu kilichoko Chakechake Pemba kwa gharama ya shilingi 223,440,000.
(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kulipa deni hilo tangu 2012 hadi leo hii?
(b) Je, Serikali inayo taarifa kwamba mwenye kampuni hiyo aliyejenga vituo hivyo amepata maradhi makubwa huku akihangaika kufuatilia haki yake hiyo bila mafanikio?
(c) Je, ni lini Serikali itamtembelea na kumpa pole kwa maradhi hayo mabaya yaliyompata?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jaku Hashimu Ayoub, kama ifuatavyo:-
(i) Mheshimiwa Mwenyekiti, mkandarasi aliyejenga Kituo cha Polisi Mkokotoni kupitia Kampuni ya Al Batna Building Co. Ltd. alishalipwa shilingi za Kitanzania 560,000,000 na anadai shilingi za Kitanzania 525,000,000 ili kumalizia ujenzi katika kituo hicho. Deni hilo limehakikiwa na Mkaguzi Mkuu wa Ndani na atalipwa mara fedha zitakapokuwa zimetolewa.
(ii) Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Serikali nitoe pole kwa mkandarasi wetu kwa maradhi yaliyompata na nimhakikishie kuwa deni lake atalipwa na Serikali iliamua kusitisha malipo kwa Wazabuni wote katika kipindi fulani kwa ajili ya kufanya uhakiki ili kuepuka kulipa madeni mara mbili.
(iii) Mheshimiwa Mwenyekiti, tutamtembelea kumpa pole baada ya kumalizika kwa Mkutano huu wa Bunge lako Tukufu kwa kadri ya upatikanaji wa nafasi.