Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 35 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 282 2017-05-26

Name

Magdalena Hamis Sakaya

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Kaliua

Primary Question

MHE. MAGDALENA H. SAKAYA aliuliza:-
Kwa kuwa lengo la Serikali kuruhusu vyombo vya usafiri wa pikipiki kubeba abiria na mizigo ni kusaidia kurahisisha usafiri na pia kutoa ajira kwa vijana hapa nchini lakini ajali zinazotokana na vyombo hivi kwa sasa ni nyingi kuliko vyombo vingine.
(a) Je, Serikali inaweza kueleza ni ajali ngapi za bodaboda zimetokea kwa miaka mitatu toka mwaka 2015
- 2017 na ni watu wangapi wamepoteza maisha kwenye ajali hizo na walemavu ni wangapi?
(b) Je, Serikali ina mikakati gani ya uhakika ya kuokoa maisha na nguvukazi ya Taifa inayopotea kwa usafiri huu?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Magdalena Sakaya, Mbunge wa Kaliua, kama ifuatavyo:-
(i) Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kipindi cha miaka mitatu toka Januari, 2015 hadi Februari, 2017 jumla ya ajali 5,418 za bodaboda zilitokea na kusababisha vifo vya watu 1,945 na majeruhi 4,696.
(ii) Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Jeshi la Polisi inayo mikakati ya kukokoa maisha na nguvu kazi ya Taifa inayopotea kutokana na ajali za bodaboda. Mikakati hiyo ni pamoja na:-
(a) Kupitishwa kwa Kanuni ya Leseni za Pikipiki na Bajaji iliyopita mwaka 2009;
(b) kutoa elimu ya Usalama Barabarani mashuleni na kupitia vipindi vya redio, televisheni pamoja na vipeperushi;
(c) Kufanya ukaguzi wa mara kwa mara kwa waendesha bodaboda;
(d) Kuimarisha usimamizi wa Sheria za Barabarani;
(e) Kusisitiza madereva wa bodaboda kuepuka kuendesha kwa mwendo kasi;
(f) Kuchukua hatua kwa vitendo vyote vya ulevi na kuweka viakisi mwanga (reflectors) ili kuonekana kwa urahisi; na
(g) Kusisitiza matumizi ya kofia ngumu ili kupunguza madhara punde ajali zinapojitokeza.