Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 36 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 294 2017-05-29

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza:-
Jimbo la Kalambo lina kata 23 na vijiji 111; katika awamu ya kwanza na ya pili ya mradi wa REA ni vijiji vichache tu vilipata umeme.
Je, katika utekelezaji wa REA III ni vijiji vingapi vinategemea kupata umeme ili wananchi wa maeneo hayo waweze kujiandaa kujiendeleza kiuchumi?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Josephat Sinkamba Kandege, Mbunge wa Kalambo, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa mradi kabambe wa usambazaji umeme vijijini awamu ya tatu umeanza rasmi tangu mwezi Machi, 2017. Mradi huu utajumuisha vipengele mradi vitatu vya densification, grid extension pamoja na off- grid renewable vinavyolenga kuongeza wigo wa usambazaji katika vijiji vyote vilivyobaki nchi nzima, vitongoji vyote, taasisi za umma, na maeneo ya pembezoni ambayo hayajafikiwa na miundombinu ya umeme. Mradi wa REA Awamu ya Tatu katika jimbo la Kalambo utajumuisha vijiji 89 kupitia vipengele
- mradi vya densification grid extension, utaokamilika mwaka 2020/2021.
Mheshimiwa Spika, kazi ya kupeleka umeme kwenye maeneo ya vijiji hivyo itajumuisha ujenzi wa njia ya msongo umeme wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilometa 413.49; ujenzi wa njia ya umeme msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilometa 745; pamoja na ufungaji wa transfoma 149. Kazi nyingine itakuwa ni kuwaunganishia umeme wateja wa awali 9,816 kazi ya gharama hii ni shilingi bilioni 36.