Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 37 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 303 2017-05-30

Name

Lameck Okambo Airo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

KITETO Z. KOSHUMA (K.n.y. MHE. LAMECK O. AIRO) aliuliza:-
Wavuvi wa Wilaya ya Rorya wanaovua katika Ziwa Victoria wamekuwa wakitekwa, kunyang’anywa nyavu zao pamoja na injini za boti. Aidha, majambazi wanaofanya vitendo hivyo hutumia silaha nzito na inasemekana ni wanajeshi kutoka Uganda.
Je, Serikali ina mkakati gani wa kuongea na Serikali ya Uganda ili kukomesha uvamizi huo?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Lameck Okambo Airo, Mbunge wa Rorya, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kumekuwepo na matukio ya uporaji wa nyavu na injini za wavuvi katika Ziwa Victoria. Uporaji huu unafanywa na wahalifu ambao bado Jeshi la Polisi halina ushahidi kuwa wanatoka ndani au nje ya nchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kukabiliana na matukio ya uhalifu ikiwemo uporaji wa nyavu na injini za wavuvi katika Ziwa Victoria, Serikali kupitia Jeshi la Polisi ina mikakati ya kununua boti zenye uwezo na zenye mwendo kasi mkubwa. Boti hizi zitasaidia askari polisi kufanya doria za mara kwa mara na kufika kwenye matukio haraka. Aidha, Serikali inashirikiana na nchi jirani katika udhibiti wa pamoja kwa matukio ya uhalifu wa majini.