Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 38 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 308 2017-05-31

Name

Allan Joseph Kiula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. ALLAN J. KIULA aliuliza:-
Wilaya ya Mkalama ni mpya na haina vitendea kazi kama vile magari katika katika Idara ya Afya na huduma za dharura zinapatikana makao makuu huku tarafa zikiwa zimetawanyika hivyo wananchi hasa wajawazito na watoto wamekuwa wakipoteza maisha kabla ya kufika hospitali kwa kukosa usafiri.
Je, ni lini Serikali itatoa gari la wagonjwa (ambulance) tatu kwa kila tarafa ikiwemo Makao Makuu ili kunusuru vifo hivyo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais –TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Allan Kiula, Mbunge wa Iramba Mashariki, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama ina gari moja la kuhudumia wagonjwa lenye usajili wa namba SM 4263 ambalo lipo katika Kituo cha Afya Kinyangiri. Kwa sasa Halmashauri imeandaa mpango wa kuwashirikisha wadau mbalimbali ili kupata gari la wagonjwa katika Kituo cha Afya cha Nyamburi ambacho kimewekwa katika mpango wa kufanyiwa ukarabati mkubwa kuwezesha huduma za upasuaji kutolewa.
Aidha, Serikali imepanga kuimarisha vituo vya afya na zahanati ili ziwe na uwezo wa kutoa huduma kwa wagonjwa wengi na kupunguza rufaa kwenda katika Hospitali ya Wilaya. Ofisi ya Rais, TAMISEMI itatoa ushirikiano wake pale Halmashauri hiyo itakapoweka kipaumbele katika kutenga fedha kupitia mapato ya ndani kwa ajili ya ununuzi wa gari la wagonjwa katika eneo hilo.