Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 9 Sitting 2 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 25 2017-11-08

Name

Raphael Michael Japhary

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL aliuliza:-
Gereza la Karanga ni chakavu na lina uhaba wa samani:-
(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kulikarabati gereza hilo?
(b) Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka fedha za kutosha za uendeshaji ili kununua samani pamoja na vifaa vingine vitakavyosaidia kutoa huduma kwa wafungwa na mahabusu gerezani hapo?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Raphael Japhary Michael, Mbunge wa Moshi Vijijini, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
– Mheshimiwa Mwenyekiti, nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge kwamba Gereza la Karanga linakabiliwa na uchakavu wa miundombinu na hali hiyo imetokana na majengo na miundombinu ya gereza hilo kuwa ya tangu mwaka 1949 likiwa na uwezo wa kuhifadhi wahalifu 814 na wahalifu waliopo sasa ni takriban 1,200. Katika kukabiliana na changamoto hiyo, Serikali inatekeleza mpango wa muda mrefu wa kuyaboresha majengo hayo kwa kuyafanyia ukarabati mkubwa unaolenga kuyaimarisha na kuyaboresha pamoja na kuyafanyia upanuzi.
– Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa na mpango wa kupeleka fedha za maendeleo kwa ajili ya ukarabati na ununuzi wa samani katika magereza yote nchini likiwemo Gereza la Karanga. Aidha, kutokana na ufinyu wa bajeti, fedha hizo zimekuwa zikitolewa kwa awamu katika magereza mbalimbali nchini.