Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 9 Sitting 4 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 51 2017-11-10

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Primary Question

MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA (K.n.y. MHE. RIDHIWANI J. KIKWETE) aliuliza:-
Maeneo ya Munguatosha na Hondogo ni baadhi ya maeneo ambayo yanahitaji transfoma ili umeme uwake.
Je, Serikali ina mpango gani juu ya kupeleka transfoma katika maeneo hayo?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ridhiwani Jakaya Kikwete, Mbunge wa Chalinze kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kijiji cha Hondogo kimewekwa katika mradi wa REA Awamu ya III kupitia Mradi wa Densification Awamu ya Kwanza ulioanza mwezi Machi, 2017 unaotekelezwa na kampuni ya STEG. Mkandarasi tayari amesimamisha nguzo 111 na kuvuta waya wenye urefu wa kilometa 4.5. Hatua inayofuata ni ufungaji wa transfoma yenye uwezo wa kVA 50 itakayofanyika mwishoni mwaka mwezi Novemba, 2017. Wateja wapatao 65 wanatarajiwa kuunganishiwa umeme.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kitongoji cha Munguatosha kilichopo katika Kijiji cha Makore kimejumuishwa na kitapatiwa umeme kupitia REA awamu ya III chini ya Grid extension utakaotekelezwa na kampuni ya Sengerema Engineering Group Limited.
Kazi ya kupeleka umeme katika Kitongoji cha Munguatosa inajumuisha ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilometa mbili, ufungaji wa transfoma yenye uwezo wa kVA 50 pamoja na kuunganisha wateja wapatao 46. Utekelezaji wa mradi huu ulianza mwezi Julai, 2017 na utakamilika mwezi Juni, 2019.