Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 9 Sitting 5 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 61 2017-11-13

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE aliuliza:-
Sekta binafsi ya ulinzi ilianzishwa mwaka 1980 ikiwa na kampuni mbili tu na ikiwa haina miongozo yoyote.
• Kwa kuwa sasa sekta hii ina kampuni zaidi ya 850 nchini kote, je, Serikali italeta Sheria ya Sekta Binafsi ya Ulinzi ili pia kuanzisha mamlaka ya sekta binafsi ya ulinzi?
• Je, Ofisi ya Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) ina mpango gani wa kushirikiana na Chama cha Sekta Binafsi ya Ulinzi ili kuimarisha ulinzi wa raia na mali zao?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Almas Athumani Maige, Mbunge wa Tabora Kaskazini, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba sekta ya ulinzi binafsi imekuwa sana hapa nchini na kwamba Serikali inatambua umuhimu wa sekta hii na ilishaanza maandalizi ya kuwasilisha Muswada wa Sheria ya Makampuni Binafsi ya Ulinzi. Katika kufanikisha jambo hili Wizara ya Mambo ya Mambo ya Ndani ya Nchi iliandaa walaka kupeleka Baraza la Mawaziri kwa hatua za awali. Ili kukamilisha hatua hii yanahitajika maoni ya wadau kutoka pande mbili za Muungano. Serikali imeweka utaratibu wa kupata maoni kutoka katika Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na mara yatakapopokelewa waraka huu utawasilishwa mapema iwezekanavyo.
(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, Ofisi ya Inspekta Jenerali wa Polisi imekuwa ikishikiana na sekta binafsi ya ulinzi katika nyanja mbalimbali. Kwa mujibu wa Sheria ya Jeshi la Polisi na Polisi Wasaidizi Namba 322 Rejeo la mwaka 2002. Jeshi la polisi limekuwa likitoa mafunzo kwa makampuni binafsi ya ulinzi, kufanya ukaguzi kuchukua alama za vidole kwa watumishi, kutoa vitambulisho na kutoa ushauri kwa makampuni hayo ili kuboresha na kuhakikisha huduma ya ulinzi inatolewa katika viwango vinavyostahili.