Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 9 Sitting 6 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 71 2017-11-14

Name

Eng. James Fransis Mbatia

Sex

Male

Party

NCCR-Mageuzi

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. JAMES F. MBATIA aliuliza:-
Sheria ya Maslahi na Mafao ya Majaji Namba tatu (3) ya Mwaka 2007 Kifungu cha 8; inafafanua kuwa Jaji Mkuu, Jaji wa Mahakama ya Rufani, Jaji Kiongozi au Jaji wa Mahakama Kuu akifariki dunia akiwa madarakani au baada ya kustaafu, Serikali itagharamia gharama za mazishi na Kifungu cha 10 cha Sheria hiyo kinafafanua malipo ya pensheni na huduma nyingine atakazostahili Jaji wakati wa kustaafu kama ilivyo kwenye Kifungu cha 20 na 21 cha Sheria ya Utumishi wa Umma:-
Je, Serikali haioni busara kuifanyia marekebisho sheria hiyo au vinginevyo ili Majaji waweze kupatiwa huduma muhimu na hasa matibabu wakati wanapostaafu?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (K.n.y. WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Katiba na Sheria, napenda kujibu swali la Mheshimiwa James Francis Mbatia, Mbunge wa Vunjo, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Sheria ya Malipo ya Mshahara na Mafao ya Hitimisho la Kazi kwa Majaji (The Judges Renumeration and Terminal Benefits Act) na Namba tatu (3) ya Mwaka 2007 katika Kifungu cha 10 na Vifungu vya 20 na 21 vya Sheria ya Mafao Katika Utumishi wa Umma (The Public Service Retirement Benefits Act) Sura ya 371 zinaweka utaratibu wa mafao na stahili za Majaji baada ya kustaafu.
Mheshimiwa Naibu Spika, masharti ya kazi na stahili za Majaji, kwa maana ya Jaji Mkuu, Majaji wa Mahakama ya Rufani, Jaji Kiongozi na Majaji wa Mahakama Kuu yamefafanua kuwa, Majaji hao wamejumuishwa katika utaratibu wa matibabu kupitia Mfuko wa Taifa wa Bima ya afya wawapo kazini na gharama hizo hulipwa na Serikali na hata wanapostaafu wanaendelea kupata huduma hizo kupitia Mfuko huo. Kwa wale waliostaafu kabla ya masharti hayo kuanza kutumika hawanufaiki na Mfuko huo.