Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 9 Sitting 8 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 104 2017-11-16

Name

Philipo Augustino Mulugo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songwe

Primary Question

MHE. PHILLIPO A. MULUGO aliuliza:-
Ziwa Rukwa lina wanyama wengi aina ya mamba waliofugwa humo ambao husababisha vifo kwa wananchi waishio pembezoni mwa ziwa hilo, wakiwemo wananchi wa Songwe na Serikali imekuwa ikitoa vibali vichache kuvuna mamba hao:-
(a) Je, kwa nini Serikali isiongeze idadi ya kuvuna mamba hao ili kuwapunguza?
(b) Kwa kuwa vifo vingi vya wakazi wa maeneo hayo vinatokana na kuliwa na mamba na Serikali haitoi mkono wa pole kwa wananchi walioathirika na vifo hivyo; je, Serikali haioni haja ya kuwafikiria wafiwa hao?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimwa Philipo Augustino Mulugo, Mbunge wa Songwe, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja, kama ifuatavyo:
Mheshimiwa Spika, uwindaji wa mamba katika mbalimbali nchini hufanyika kwa kuzingatia takwimu kuhusu idadi ya mamba kwa mujibu wa sensa zinazofanywa katika maeneo husika. Lengo la uwindaji wa mamba ni pamoja na kupunguza madhara yanayosababishwa na wanyama hao kwa wananchi.
Mheshimiwa Spika, Wizara yangu kupitia taasisi ya utafiti wa wanyama pori Tanzania TAWIRI, imepanga kufanya sensa ya mamba na viboko kwa nchi nzima kwa mwaka wa fedha 2017/2018. Sensa hii inalenga kubaini idadi ya wanyama hao ili kuwezesha upangaji wa mgao utakaovumwa. Maeneo yatakayohusika katika sensa hii, ni maeneo ya maziwa na mito yote ikiwemo Ziwa Rukwa ambako kwa sasa inaonekana kuwa na tatizo la mamba.
Mheshimiwa Spika, Wizara yangu hufanya malipo ya kifuta machozi na jasho kwa wahanga baada ya kupata taarifa zenye takwimu ya matukio ya wananchi kuuawa au kujeruhiwa na mamba kutoka kwenye maeneo husika. Malipo hayo hufanyika kwa mujibu wa Sheria ya Kuhifadhi Wanyamapori Na. 5 ya mwaka 2009 na kanuni za kifuta jasho na machozi za mwaka 2011. Aidha, malipo hayo hayawahusu watu waliopoteza maisha au kujeruhiwa wakati wakifanya shughuli ambazo haziruhusiwi kisheria kwa mujibu wa kifungu cha 71(3) cha Sheria ya Kuhifadhi Wanyamapori Na. 5 ya mwaka 2009.
Mheshimiwa Spika, Wizara yangu imeandaa mikakati ya muda mfupi na muda mrefu ya kukabiliana na wanyama pori wakali wakiwemo mamba katika Ziwa Rukwa…..
Mheshimiwa Spika, napenda kutoa rai kwa Waheshimiwa Wabunge na Mamlaka za Wilaya husika ili ziwasilishe nyaraka zinazothibitisha wananchi kuathirika na wanyamapori wakali ili Serikali iweze kuchua hatua sitahiki.