Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 9 Sitting 9 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 114 2017-11-17

Name

Nuru Awadh Bafadhili

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NURU A. BAFADHILI aliuliza:-
Askari Polisi wengi katika Jiji la Tanga wanaishi uraiani ambapo ni kinyume cha maadili kutokana na ukosefu wa nyumba za kuishi katika kambi zao.
• Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga upya nyumba za askari hao?
• Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwajengea nyumba za ghorofa askari wa Kambi za Chumbageni, Mabawa na Madina Msambweni, ili ziweze kuwaweka askari wengi katika eneo moja, kama ilivyo Kilwa Road Dar es Salaam?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Nuru Awadh Bafadhili, Mbunge wa Viti Maalum, lenye kipengele (a) na (b) kwa pamoja kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua uchakavu wa nyumba za kuishi askari katika Jiji la Tanga na maeneo mengine hapa nchini. Katika kukabiliana na tatizo la uchakavu na upungufu wa nyumba za kuishi askari polisi, Serikali ina mpango wa kujenga nyumba mpya katika Jiji la Tanga na maeneo mengine kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaona umuhimu wa kujenga nyumba za ghorofa kwa ajili ya makazi ya askari, kama ilivyojenga nyumba za Kilwa Road Jijini Dar es Salaam, Ziwani kwa upande wa Zanzibar pamoja na Buyekela Mwanza kwa kuwa zina uwezo wa kuchukua familia nyingi katika eneo dogo la ardhi. Aidha, taratibu za ujenzi wa nyumba za kuishi askari polisi Jijini Tanga zitakapoanza wataalam watazingatia ushauri wa Mheshimiwa Mbunge.