Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 10 Sitting 1 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 06 2018-01-30

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza:-
Katika Mtaa wa Mongolandege, Kata ya Ukonga, kuna daraja la Mongolandege ambalo huunganisha Jimbo la Ukonga na Jimbo la Segerea. Aidha, daraja la Mto Nyebulu huunganisha Kata ya Buyuni na Kata ya Chanika Magengeni.
Je, ni lini Serikali itajenga madaraja hayo muhimu ili kurahisisha huduma za kijamii katika maeneo yaliyotajwa?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwita Mwikabe Waitara, Mbunge wa Ukonga, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, daraja la Mongolandege linatakiwa kujengwa katika Bonde la Mto Mzinga ambalo awali palijengwa makalavati kwa nguvu za wananchi. Kalavati hizo zilishindwa kufanya kazi kwa ufanisi baada ya mkondo wa mto kupanuka.
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, mwaka 2012, Manispaa ya Ilala ilijenga box culvert ili kuwezesha eneo hilo kupitika. Hata hivyo, mvua zilizonyesha kwa wingi katika kipindi hicho zilileta madhara makubwa ambapo bonde hilo lilitanuka na kalavati hiyo kusombwa na maji na kusababisha kukosekana mawasiliano katika eneo hilo. Daraja la Nyebulu linatakiwa kujengwa katika Mto Vikorongo na litakuwa na wastani wa upana wa mita 30.
Mheshimiwa Naibu Spika, TARURA katika Halmashauri ya Manispaa ya Ilala itatenga fedha katika mpango wa matengenezo ya barabara na madaraja kwa mwaka wa fedha 2018/2019 za kufanyia usanifu wa kina kwa ajili ya madaraja yote mawili. Aidha, baada ya usanifu huo kukamilika, gharama halisi za ujenzi wa madaraja hayo zitafahamika na kutengwa kwenye bajeti.