Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 10 Sitting 1 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 15 2018-01-30

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza:-
Je, ni lini Wilaya ya Lushoto itaanza tena kupokea matangazo ya Redio ya Taifa (TBC)?

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, napenda kujibu la Mheshimiwa Rashid Abdallah Shangazi, Mbunge wa Mlalo, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kijiografia Wilaya ya Lushoto katika Mkoa wa Tanga ni kati ya Wilaya ambazo zinazozungukwa na milima, mazingira ambayo huzuia mawimbi ya TBC FM pamoja na TBC Taifa, ambayo hurushwa kutokea mitambo ya FM iliyoko katika eneo la Mnyuzi Wilayani Muheza.
Mheshimiwa Naibu Spika, ili kutatua changamoto hii, TBC imeamua sasa mtambo wa kurushia matangazo hayo ujengwe katika Wilaya ya Lushoto ili matangazo ya redio yaweze kufika kwa uhakika katika wilaya hii. Ili kufanikisha kazi hii, TBC imetenga shilingi milioni 50 toka bajeti yake ya ndani kwa ajili ya mnara utakaotumika kuweka mtambo wenye nguvu ya watt 500 na viunganishi vyake kwa ajili ya kupokea matangazo hayo. Mtambo huu utafungwa katika eneo la Kwemashai ambako kuna miundombinu ya kuwezesha zoezi hili kukamika kabla ya mwisho wa mwaka huu wa fedha.