Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 10 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 16 2018-01-31

Name

Silvestry Fransis Koka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Mjini

Primary Question

MHE. SILVESTRY F. KOKA aliuliza:-
Mji wa Kibaha ni Makao Makuu ya Mkoa wa Pwani na yapo maombi yaliyokwishapelekwa Serikalini kuomba Mji huo upewe hadhi ya kuwa Manispaa lakini hakuna majibu kwa ombi hilo hadi sasa:-
Je, ni kwa nini mpaka sasa Serikali haijaupa hadhi Mji huo kuwa Manispaa?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Silvestry Francis Koka, Mbunge wa Kibaha Mjini kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya maombi ya kuupandisha hadhi Mji wa Kibaha kuwa Manispaa kupokelewa mwezi Agosti, 2016; Ofisi ya Rais , TAMISEMI ilifanya uhakiki uliobaini kuwa Mji wa Kibaha ulikuwa na wakazi 128,488 (sensa ya Mwaka 2012), Kata 14, Mitaa 73 ambapo ni asilimia 56 tu ya wakazi ndio walikuwa wakipata huduma za maji safi na pia haukuwa na mpango kabambe wa uendelezaji wa Mji (Master plan).
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa mwongozo wa Serikali wa mwaka 2014, vigezo vya kupandisha hadhi miji kuwa manispaa unatakiwa kuwa na wakazi si chini ya 300,000, Kata si chini ya 15, Mitaa si chini ya 75, wakazi wanaopata huduma za maji wawe si chini ya asilimia 75 ya wakazi wote wa mji na uwepo mpango kabambe wa uendelezaji wa Mji (Master plan). Kutokana na vigezo hivyo kutofikiwa, ilidhihirika kuwa Mji wa kibaha haukuwa umefuzu kupandishwa hadhi kuwa Manispaa. Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani alijulishwa matokeo hayo kwa barua yenye kumb. Na. CCB.132/394/01/16 ya tarehe 12 Juni, 2017.