Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 10 Sitting 2 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 23 2018-01-31

Name

Prof. Jumanne Abdallah Maghembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Primary Question

MHE. PROF. JUMANNE A. MAGHEMBE aliuliza:-
Miradi ya REA I na II katika Wilaya ya Mwanga haikukamilika na fedha zilizokuwa zimepangwa hazikutumika:-
(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia umeme wananchi waliopitiwa na umeme huo bila kufungiwa?
(b) Je, Awamu ya III ya REA iliyozinduliwa Mwanga, mwezi Septemba, 2017 itaanza kutekelezwa lini?
elezaji wa REA Awamu ya I na II Wilaya ya Mwanga
MHE. PROF. JUMANNE A. MAGHEMBE aliuliza:-
Miradi ya REA I na II katika Wilaya ya Mwanga haikukamilika na fedha zilizokuwa zimepangwa hazikutumika:-
(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia umeme wananchi waliopitiwa na umeme huo bila kufungiwa?
(b) Je, Awamu ya III ya REA iliyozinduliwa Mwanga, mwezi Septemba, 2017 itaanza kutekelezwa lini?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Profesa Jumanne Abdallah Maghembe, Mbunge wa Mwanga, lenye Sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, jumla ya vijiji 38 kati ya vijiji 44 vya Wilaya ya Mwanga vilipata umeme kupitia Awamu ya II ya Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini ambapo wateja zaidi ya 2,241 waliunganishiwa umeme. Aidha, vijiji sita vilivyosalia havikuweza kupatiwa umeme kutokana na Mkandarasi, Kampuni ya SPENCON, aliyekuwa anafanya kazi hiyo kushindwa kukamilisha kazi hiyo na mkataba wake kusitishwa mwezi Disemba, 2016.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imempata Mkandarasi Kampuni ya M/S Octopus Engineering Limited atakayeikamilisha kazi ya kupeleka umeme katika vijiji vilivyosalia kwa awamu ya pili. Kazi hizo zimeanza rasmi mwezi Januari, 2018 na zitakamilika ndani ya miezi sita.
Mheshimiwa Mwenyekiti, utekelezaji wa Mradi wa REA Awamu ya Tatu katika Wilaya ya Mwanga ulianza mwezi Oktoba, 2017 chini ya Mkandarasi Kampuni ya Urban and Rural Engineering Services Limited. Kazi za mradi zinahusisha ujenzi wa njia ya umeme msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilometa 10.98; njia ya umeme msongo wa kilovoti 0.4 urefu wa kilometa 24; ufungaji wa transformer 12 za kVA 50; pamoja na kuunganisha wateja wa awali 347. Gharama za mradi ni Dola za Marekani milioni 1.7 na shilingi bilioni 12.3; mradi huu utakamilika mwezi Juni, 2021.