Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 10 Sitting 3 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 35 2018-02-01

Name

Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Mkoa wa Katavi?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA VIJANA (K.n.y. WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Anna Richard Lupembe, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imejiwekea mpango mkakati wa kujenga Mahakama katika Mikoa na Wilaya zote nchini kwa awamu. Katika mpango huu, Mahakama ya Mkoa wa Katavi ambalo jengo lake litakuwa pia ni Mahakama ya Wilaya ya Mpanda lilipangwa kujengwa katka mwaka wa fedha wa 2017/2018.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tayari ujenzi umekwishakuanza na unatarajia kukamilika kabla ya Juni 2018. Aidha, huu ni moja ya miradi ya ujenzi wa Mahakama inayotekelezwa nchini kwa kutumia teknolojia rahisi na ya kisasa ya moladi.