Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 10 Sitting 5 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 68 2018-02-05

Name

Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. MWANNE I. MCHEMBA aliuliza:-
Hali ya nyumba za Polisi na Magereza nchini ni mbovu sana. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga nyumba za askari hao?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mwanne Ismail Mchemba, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli hali ya makazi kwa Askari wetu siyo nzuri, hata hivyo Serikali imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo na kwa kutumia rasilimali zilizopo katika maeneo husika kujenga makazi mapya na kufanya ukarabati wa majengo yaliyopo.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika bajeti ya mwaka 2017/2018 Serikali imetenga jumla ya shilingi bilioni 12.3 fedha za maendeleo kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa makazi ya askari wetu katika maeneo mbalimbali nchini.