Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 6 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 74 2018-02-06

Name

Juma Kombo Hamad

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Wingwi

Primary Question

MHE. JUMA KOMBO HAMAD aliuliza:-
Kumekuwa na mgongano mkubwa wa Katiba kati ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Katiba ya Zanzibar unaosababisha ongezeko la Kero za Muungano na mgongano wa kimamlaka baina ya Serikali mbili:-
Je, ni lini Serikali ya Muungano italeta mapendekezo ya mabadiliko ya Katiba ili kuondoa changamoto zilizomo ndani ya Katiba hizo?

Name

Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilosa

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Juma Kombo Hamad, Mbunge wa Wingwi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kikatiba hakuna mgongano mkubwa wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Katiba ya Zanzibar unaosababisha ongezeko kubwa la Kero za Muungano wala mgongano wa kimamlaka baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeweka utaratibu mahsusi wa kushughulikia tafsiri ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano au utekelezaji wake inayobishaniwa kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Hadi sasa hakuna upande wowote baina ya Serikali hizi mbili ambao una tafsiri tofauti ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano au utekelezaji wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuzingatia kuwa, hakuna mgongano wa Katiba kati ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Katiba ya Zanzibar, Serikali haina sababu ya kuleta Mapendekezo ya Mabadiliko ya Katiba ili kuondoa changamoto hiyo ambayo haipo.