Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 10 Sitting 7 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 90 2018-02-07

Name

Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Primary Question

MHE. JOSEPH R. SELASINI aliuliza:-
Wananchi wa Kata za Mahinda, Ngoyoni, Mengwe na Kirongo – Samanga walifanya uamuzi wa kujenga vituo vya polisi kwa nguvu zao na vituo hivyo vimefikia hatua mbalimbali za ujenzi, lakini kutokana na kuwepo na shughuli nyingine zinazohitaji michango ya wananchi kama vile ujenzi wa vituo vya afya, zahanati na maabara wameshindwa kumalizia vituo hivyo.
Je, Serikali iko tayari kuchukua hatua za kumalizia ujenzi wa vituo hivyo njia ya kuwatia moyo wananchi?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Roman Selasini, Mbunge wa Rombo kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba kupongeza sana juhudi za wananchi wa Mahida, Ngoyoni, Mengwe na Korongo kwa uamuzi wao wa kujenga vituo vya polisi kwa nguvu zao wenyewe. Kutokana na ujenzi wa vituo hivyo kuwa katika hatua mbalimbali. Serikali kupitia jeshi la polisi itafanya ukaguzi wa vituo hivyo ili kupata tathmini ya gharama zitakazohitajika katika kukamilisha ujenzi huo. (Makofi)