Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 10 Sitting 7 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 91 2018-02-07

Name

Julius Kalanga Laizer

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Monduli

Primary Question

MHE. JULIUS K. LAZIER aliuliza:-
Hivi karibuni Serikali ilitoa maelekezo kwa Wakuu wa Mikoa kusimamia urejeshwaji wa mashamba makubwa ambao hayakuendelea yakiwemo ya Wilaya ya Monduli.
Je, ni lini Serikali itakamilisha mchakato wa kufuta mashamba 25 katika Wilaya ya Monduli ambayo mchakato wake kwa ngazi ya Halmashauri umekamilika?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Julius Kalanga Laizer Mbunge wa Monduli kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kufuatia maelekezo ya Serikali kwa mikoa kusimamia urejeshwaji wa mashamba yasiyoendelezwa nchini, Wizara yangu imekuwa ikipokea mapendekezo ya kubatilisha miliki za mashamba na viwanja ambavyo wamiliki wake wakiuka masharti ya kumiliki ardhi kwa kutoendeleza, kutelekeza au kuendeleza kinyume na masharti au kutolipa kodi ya pango la ardhi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2015 Halmashauri ya Wilaya ya Monduli ilifanya ukaguzi kwa mashamba 25 ambayo yalikuwa hayajaendelezwa. Katika ukaguzi huo ilibainika kuwa kati ya mashamba yaliyokaguliwa, mashamba 12 hayakuwa na nyaraka kamili za umiliki, kwa maana ya barua ya toleo au hati na hivyo kutokuwa halali kwa kubatilishwa kwa mujibu wa sheria.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri iliwasilisha mapendekezo ya kufutwa mashamba 13 tu na Wizara yangu imekamilisha utaratibu wa kubatilisha miliki za mashamba hayo yote 13 yaliyopo katika maeneo ya Mswakini Juu, Lolkisale na Maserani yenye ukubwa wa jumla ya ekari 131,873.35 Mashamba haya yamerejeshwa kwa Halmashauri ya Wilaya ya Monduli chini ya usimamizi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa ajili ya kuandaliwa mpango wa matumzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, nichukue fursa hii kuwakumbusha Halmashauri kuwa maeneo yanayorejeshwa kwao wakumbuke kuwa na mpango mzuri wa matumizi ikiwepo kutenga maeneo kwa ajili ya uwekezaji pamoja na matumizi mengine ya wananchi. Hata hivyo hadi leo Wilaya na Mkoa hawajaleta mapendekezo rasmi ya kutumia ardhi hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara yangu inaendelea kupokea na kushughulikia mapendekezo ya kubatilisha milki za mashamba mengine kutoka Halmashauri mbalimbali nchini baada ya wamiliki kupewa ilani kwa mujibu wa sheria.