Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 10 Sitting 7 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 92 2018-02-07

Name

Amb. Adadi Mohamed Rajabu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Primary Question

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB aliuliza:-
Wilaya ya Muheza imetenga eneo sehemu ya Chatur kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za NHC za bei nafuu na baadae kuuziwa wananchi na NHC walishalipia eneo hilo. Je, ni lini ujenzi huo utaanza?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Balozi Adadi, Mbunge wa Muheza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Shirika la Nyumba la Taifa linatambua kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza kuna mahitaji makubwa ya nyumba. Utekelezaji wa mradi wa nyumba Muheza unakwenda sambamba na mpango wa Shirika wa kujenga nyumba za bei nafuu katika Wilaya mbalimbali hapa nchini. Kwa sasa Shirika la nyumba tayari limeingia makubaliano na Halmashauri ya Muheza ili kujenga nyumba 10 katika makubaliano yaliyofanyika tarehe 29 Septemba, 2017 baada ya Halmashauri kuridhia rasmi ramani ya nyumba ambazo zilipendekezwa. Aidha, Halmashauri imeshalipa malipo ya awali kiasi cha shilingi milioni 100 ikiwa ni sehemu ya malipo ya nyumba hizo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Shirika la Nyumba lina eneo lenye ukubwa wa ekari 83 katika eneo la Chatur. Kwa sasa watalaam wa Shirika la Nyumba wako katika eneo la mradi wakiandaa mpango wa kina kwa matumizi ya viwanja (site plan). Baada ya kukamilisha kwaundaa mpango wa kina wa matumizi ya ardhi, Shirika la Nyumba litajenga nyumba 20 kwa gharama nafuu ambapo nyumba 10 ni kwa ajili ya Halmashauri ya Wilaya ya Muheza na nyumba nyingine 10 zitauzwa kwa wananchi wengine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitoe rai kwa halmashauri nyingine kuiga mfano wa Halmashauri ya Muheza pamoja na halmashauri zingine ambazo tayari zimekwisha faidika na huduma hiyo zikiwemo Halmashauri ya Busokelo, Uyui, Momba, Geita na kwingineko ambao kwa kiasi kikubwa wamepunguza tatizo la makazi kwa wafanyakazi wao. Kwa Halmashauri ambazo zilijengewa nyumba lakini hawajanunua nyumba hizo kwa sasa soko liko wazi kwa mwananchi yeyote kununua nyumba hizo.