Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 10 Sitting 8 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 105 2018-02-08

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza:-
Ni muda mrefu tangu transfomer katika Kijiji cha Itengelo, Kata ya Saja imefungwa lakini umeme haujawashwa. Je, ni lini Serikali itawasha umeme katika kijiji hicho?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Neema William Mgaya, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Kijiji cha Itengelo ni miongoni mwa vijiji vilivyonufaika na mradi wa REA Awamu ya Pili uliotelekezwa na Mkandarasi Kampuni ya M/S Sengerema Engineering Group Limited ambaye alipewa kazi ya mradi kwa Mkoa wa Njombe. Kazi zilizofanyika ni pamoja na ujenzi wa kilometa 8.5 za njia za umeme msongo wa kilovoti 33 na kilometa sita za njia za umeme msongo kilovoti kwa gharama ya shilingi milioni 564. Maradi ulikamilika mwezi Desemba, 2016.
Mheshimiwa Naibu Spika, Kijiji cha Itengelo kiliwashiwa umeme tarehe 22/08/2017 kwa kufungiwa transfomer mbili pamoja na kuwaunganisha umeme wateja 56 waliolipia.