Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 10 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 109 2018-02-09

Name

Prof. Norman Adamson Sigalla King

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. PROF. NORMAN A. S. KING aliuliza:-
Mwaka 2013 Serikali ilianza kutekeleza mradi wa maji wa Kata za Kinyika na Matamba katika Wilaya ya Makete lakini mradi huo haukufanikiwa kutokana na Serikali kutoa maelekezo ya kulaza mabomba ya inchi 2.5 na 4 badala ya inchi 8 kwenye mradi wa kilometa 18; mradi wa maji wa Tarafa za Magoma na Bulongwa ulijengwa muda mrefu wakati idadi ya watu ikiwa ndogo lakini sasa idadi ya watu na matumizi vimeongezeka.
(a) Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa mradi wa maji wa Tarafa ya Matamba?
(b) Je, ni lini Serikali itakamilisha mradi wa maji wa Tarafa ya Bulongwa ili Kata za Bulongwa, Kipagalo na Luwumbu ziweze kupata maji?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Norman Sigalla King, Mbunge wa Makete lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, mradi wa maji wa Kata ya Matamba na Kinyika unaosambaza huduma za maji kwenye vijiji tisa ulianza kujengwa mwaka 2007 na ulikamilika mwaka 2014. Kabla ya ujenzi kuanza usanifu wa mradi huo ulilazimika kubadilishwa ili kutumia bomba la inchi 4, 2 na 1.5 badala ya bomba la inchi 8 kulingana na fedha zilizokuwepo kwani gharama za mradi kwa usanifu wa awali zilikuwa kubwa zaidi. Kutokana na ongezeko la watu kutoka 12,019 mwaka 2007 hadi 17,686 kwa sasa mradi huo haukidhi mahitaji. Ili kukidhi mahitaji Serikali inakamilisha usanifu wa mradi utakaotoa maji Mto Misi ambapo ujenzi unatarajiwa kuanza mwaka 2018/2019.
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba mradi wa maji Bulongwa na Magoma unaohudumia vijiji 14 uliojengwa mwaka 1984 haukukidhi mahitaji ya sasa na miundombinu yake ni chakavu. Serikali imeanza ukarabati wa mradi ambapo hadi sasa bomba jipya kwa umbali wa kilometa nne limelazwa na linahudumia Vijiji vya Unyangogo, Iniho na Mwakauta. Mchakato wa kumpata mkandarasi atakayetekeleza awamu ya pili ya ukarabati huo unaendelea ili kukarabati bomba kwa umbali wa kilometa mbili. Ukarabati wa mradi mzima unatarajiwa kukamilika ifikapo Juni 30, 2018.