Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 10 Sitting 9 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 120 2018-02-09

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Primary Question

MHE. OMARY T. MGUMBA aliuliza:-
Kata sita za Tegetelo, Kibuko, Tomondo, Tununguo, Seregete, Matuli na Mkulazi katika Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki hazijafikiwa na miundombinu ya umeme mpaka sasa. Je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika kata hizo?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Omary Tebweta Mgumba, Mbunge wa Morogoro Kusini Mashariki, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, lengo la Serikali ni kufikisha umeme katika vijiji vyote visivyo na umeme nchini ikiwemo vijiji vya Wilaya ya Morogoro ifikapo mwezi Juni, 2019. Kupitia mzunguko wa kwanza wa awamu ya tatu ya miradi ya kusambaza umeme vijijini katika Wilaya ya Morogoro vijiji 14 vitapatiwa umeme ifikapo mwezi Aprili, 2019. Vijiji hivyo ni pamoja na Tununguo, Kibwege, Lung’ala, Kidugalo, Kinonko, Vihengele, Konde, Vigolegole, Singisa, Rudewa, Bonye, Mtego wa Simba, Muungano na Mangala.
Mheshimiwa Naibu Spika, kazi za kupeleka umeme katika vijiji hivyo, zinajumuisha ujenzi wa kilometa 16.5 za njia za umeme msongo wa kilovolti 33 na kilometa 16 za njia za umeme msongo kilovolti 0.4, kufunga transfomer nane na kuunganisha wateja 258. Gharama ya mradi inakadiriwa kuwa shilingi bilioni 1.3. Kazi hii itatekelezwa na Mkandarasi Kampuni ya State Grid Electrical and Technical Works.
Mheshimiwa Naibu Spika, vijiji vitakavyobaki katika mzunguko wa kwanza wa REA Awamu ya Tatu vitapatiwa umeme katika mzunguko wa pili wa REA Awamu ya Tatu ambapo mradi unategemewa kuanza mwezi Julai, 2019 na kukamilika mwezi Juni, 2021.