Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 1 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 08 2018-04-03

Name

Dr. Ally Yusuf Suleiman

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mgogoni

Primary Question

MHE. DKT. SULEIMAN ALLY YUSSUF aliuliza:-
Kuna ushahidi wa kutosha kwamba kuna watu kadhaa ambao wamekuwa wakikamatwa na Jeshi la Polisi Unguja na Pemba huku baadhi yao wakifunguliwa mashtaka na wengine kuachiwa:-
(a) Je, ni kwa nini Jeshi la Polisi linashindwa kufanya kazi kwa weledi na kukamata watu pasipo ushahidi kwa lengo la kukomoa tu?
(b) Ili kulisafisha Jeshi la Polisi, je, Serikali haioni haja ya kuwawajibisha watendaji ambao wenye tabia ya kuwakomoa wananchi kwa kuwakamata pasipo ushahidi?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Dkt. Suleiman Ally Yussuf, Mbunge wa Mgogoni, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Jeshi la Polisi ni chombo kilichoundwa kwa mujibu wa Katiba na Sheria na linatekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Katiba na Sheria na kanuni na taratibu zilizopo, jukumu lake kuu likiwa ni kulinda usalama wa raia na mali zao. Jeshi la Polisi limepewa mamlaka ya kisheria ya kukamata, kuhoji na kuweka watuhumiwa mahabusu kwa muda ulioruhusiwa kisheria endapo itabainika kuwa kuna viashiria au taarifa ya kuhusika katika kutenda kosa la jinai.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa sheria na kanuni na taratibu za utendaji zinazoongoza Jeshi la Polisi linapobainika askari amebambika kesi kwa sababu zozote zile huchukuliwa hatua mbalimbali za kinidhamu ikiwamo kufukuzwa kazi.