Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 43 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 350 2017-06-07

Name

John Peter Kadutu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. GEORGE M. LUBELEJE ( K.n.y MHE. JOHN P. KADUTU) aliuliza:-
Kumekuwa na maombi ya kupata Wilaya na Halmashauri ya Ulyankulu kwa muda mrefu sasa. Pia zimetolewa ahadi za kuunda Wilaya na Halmashauri tangu mwaka 2010.
(a) Je, ni lini Serikali itawapatia wananchi Wilaya na Halmashauri kwani vigezo vya kuwa Wilaya/Halmashauri ni kama vile vya Jimbo ambavyo tayari vimetimia?
(b) Je, ni kikwazo gani kimesababisha kutopata Wilaya/Halmashauri mpaka sasa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa John Peter Kadutu, Mbunge wa Ulyankulu lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, maombi ya kuanzisha Wilaya ya Ulyankulu ya mwaka 2010 hayakufanikiwa kutokana na kutokidhi vigezo vikiwemo idadi ya watu pamoja na sehemu kubwa ya eneo hilo kuwa ni hifadhi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa maombi ya mwaka 2010 hayakukidhi vigezo na kwa sasa kama Halmashuari inaona eneo hilo limekidhi vigezo hivyo, tunashauri Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua kuanzisha mchakato wa kujadili mapendekezo hayo upya na kuyapitisha katika Baraza la Madiwani na Kamati ya Ushauri ya Wilaya na Mkoa na hatimaye kuwasilisha Ofisi ya Rais (TAMISEMI) ili yaweze kufanyiwa kazi. Serikali haitasita kuridhia pendekezo hilo endapo litakuwa limekidhi vigezo na taratibu zilizokuwa zimewekwa kwa mujibu wa Sheria.