Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 45 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 373 2017-06-12

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA alijibu:-
Kumekuwa na wimbi kubwa la uhalifu unaofanywa na baadhi ya madereva wa bodaboda na bajaji katika maeneo mengi Jijini Dar es Salaam.
(a) Je, Serikali mpaka sasa imechukua hatua gani kudhibiti wimbi hili linalokuwa tishio kwa watumiaji wa vyombo vya usafiri?
(b) Je, Serikali ina utaratibu gani wa kuhakiki na kutambua mmiliki, dereva na mahali zinapopaki bajaji na bodaboda?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hawa Subira Mwaifunga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kumekuwepo na ongezeko la uhalifu unaofanywa na waendesha bodaboda ama bajaji katika maeneo mengi Jijini Dar es salaam. Hata hivyo, Serikali kupitia Jeshi la Polisi imekuwa ikichukua hatua mbalimbali kama kufanya doria za magari, doria za pikipiki na za watembea kwa miguu lakini pia kuanzisha na kushirikiana na vikosi vya ulinzi shirikishi ili kubaini na kuzuia uhalifu katika maeneo ya makazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Serikali za Mitaa, Halmashauri na Jiji la Dar es Salaam imeendelea kuhakiki pikipiki hizo ikiwa ni pamoja na kuwapangia maeneo ya kuegesha (ku-park). Aidha, kupitia usajili wa TRA na Serikali za Mitaa, Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam imeendelea kuhakiki pikipiki hizo ikiwa ni pamoja na kuanzisha utaratibu wa kuzisajili katika maeneo ya maegesho ili kupata kumbukumbu za mmiliki, dereva na eneo maalum wanaloegesha pikipiki hizo.