Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 49 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 402 2017-06-16

Name

Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Primary Question

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO aliuliza:-
Mahakama ya Wilaya ya Kasulu ni ya zamani sana, ni chakavu sana na wakati mwingine huduma hazitolewi kabisa.
• Je, ni kwa nini Serikali imeitelekeza Wilaya ya Kasulu?
• Je, mahakama hiyo itajengwa lini?

Name

Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilosa

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Daniel Nicodemus Nsanzungwanko, Mbunge wa Kasulu Mjini lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa jengo la Mahakama ya Wilaya ya Kasulu ni chakavu. Hata hivyo, mpango wa Serikali kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ilikuwa ni kujenga upya jengo la Mahakama ya Wilaya ya Kasulu ambapo hadi sasa mkandarasi wa ujenzi huo ameshapatikana na anategemea kuingia makubaliano ya ujenzi huo mwishoni mwa mwezi huu wa Juni, 2017. Hivyo napenda kumuhakikishia Mheshimiwa Mbunge kuwa kwa mwaka wa fedha 2017/2018 Mahakama itaanza utetelezaji wa ujenzi wa Mahakama ya Wilaya ya Kasulu.