Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 49 Energy and Minerals Wizara ya Madini 405 2017-06-16

Name

Dr. Mary Michael Nagu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. DKT. MARY MICHAEL NAGU aliuliza:-
Serikali imetoa kiasi cha shilingi milioni mia tatu (300,000,000/=) kwa ajili ya ujenzi wa Mradi wa Maji wa Katesh, hata hivyo mradi huo bado haujaweza kuwanufaisha wananchi kwa sababu ya gharama kubwa za umeme zinazosababisha pampu za maji kufanya kazi kwa muda mfupi tu.
Je, Serikali haioni haja ya kupunguza au kuondoa kabisa tariff zilizopo ili gharama ya umeme iwe chini kidogo na kusaidia kusambaza maji kwa ufanisi?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Mary Michael Nagu, Mbunge wa Hanang, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia mradi kabambe wa REA Awamu ya Tatu inasambaza umeme vijijini kwa kuweka kipaumbele kwenye huduma za jamiii ikiwemo Mradi wa Maji wa Katesh. Lengo la Mradi huu ni kuwezesha huduma hiyo kupatikana kwa urahisi na kwa gharama nafuu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, gharama za kuendesha mtambo wa kusukuma maji kwa kutumia umeme ziko chini ukilinganisha na gharama ya kutumia mafuta ya dizeli. Gharama ya kuzalisha unit moja ya umeme ni shilingi 292 wakati gharama za kufua umeme kwa kutumia mafuta shilingi 450 hadi shilingi 800.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, gharama ya kuunganisha umeme kupitia Mradi wa REA ni shilingi 27,000 tu ambayo ni VAT kwa ajili ya Serikali kwa sababu Serikali imegharamia kwa asilimia 100.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa gharama za umeme ni nafuu kuliko gharama za mafuta, tunashauri Halmashauri husika itenge pesa kwa ajili ya kuunganisha umeme katika mitambo ya maji.