Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 50 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 408 2017-06-19

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. MAHMOUD H. MGIMWA (K.n.y. MHE. DEO K. SANGA) aliuliza:-
Serikali iliahidi kufuta Ushuru mdogo mdogo unaokusanywa na Halmashauri ili wajasiriamali wadogo wakiwemo akina mama lishe waweze kuongeza kipato kupitia shughuli zao.
Je, ni lini Serikali itatoa tamko rasmi kwa Halmashauri zetu nchini ili wasikusanye tena ushuru huo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deo Kasenyanda Sanga, Mbunge wa Makambako kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imefuta ushuru na tozo ambazo zilikuwa zinatozwa kwa wafanyabiashara wadogo wadogo wasio rasmi na wanaofanyia biashara katika maeneo yasiyo rasmi mfano Mama Lishe, wauza mitumba wadogo wadogo, wauza mazao ya kilimo wadogo wadogo kama mboga mboga na ndizi na matunda isipokuwa biashara za migahawa na maduka na wale ambao wako kwenye maeneo rasmi. Vilevile wafanyabiashara wadogo walio nje ya maeneo maalum ya kibiashara wenye mitaji chini ya shilingi 100,000 hawatatozwa ada, kodi na tozo zozote. Kodi nyingine zilizofutwa ni ushuru wa huduma (service levy) kwenye nyumba za kulala wageni, ada za vibali vinavyotolewa na Mamlaka za Serikali za Mitaa ambazo zilikuwa zinatozwa na TFDA, OSHA, Fire na Bodi ya Nyama na ada ya makanyagio.
Serikali pia imepunguza ushuru wa mazao kutoka asilimia tano haid asilimia mbili kwa mazao ya chakula na asilimia tatu kwa mazao ya biashara. Aidha, mazao yanayosafirishwa kutoka wilaya moja hadi nyingine yasiyozidi tani moja hayatatozwa ushuru wa mazao.