Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 52 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 426 2017-06-21

Name

Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Primary Question

MHE. KISWAGA B. DESTERY aliuliza:-
Madiwani ni wasimamizi wakuu wa rasilimali za halmashauri na wakati wa uchaguzi wa Madiwani, Wabunge na Rais ni mafiga matatu:-
• Je, ni lini Serikali itawaongezea posho ya mwezi Madiwani hao?
• Je, ni lini Serikali itawapa usafiri na msamaha wa kodi Madiwani katika vyombo vya usafiri?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Boniventura Destery Kiswaga, Mbunge wa Magu, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua kazi kubwa na nzuri inayofanywa na Waheshimiwa Madiwani katika Mamlaka za Serikali za Mitaa. Kwa Mwaka wa Fedha 2012/2013 Serikali ilipandisha posho za Madiwani kwa mwezi kutoka Sh.120,000/= hadi Sh.250,000 kupitia Waraka Maalum wa tarehe 16 Agosti, 2012. Vile vile katika Mwaka wa Fedha 2014/2015 posho hiyo iliongezwa kutoka Sh.250,000/= hadi Sh.350,000/= kwa mwezi kwa Madiwani na Sh.400,000/= kwa mwezi kwa Mwenyekiti au Meya. Serikali itaendelea kuboresha maslahi ya Waheshimiwa Madiwani kadri hali ya uchumi wa nchi inavyoruhusu.
(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la Waheshimiwa Madiwani kupewa vyombo vya usafiri na msamaha wa kodi, kwa sasa Serikali imeridhia Waheshimiwa Madiwani wakopeshwe na Mabenki kwa masharti nafuu kutokana na posho zao. Tayari mabenki yameanza kutoa mikopo kwa Waheshimwa Madiwani zikiwemo Benki za NMB na CRDB.