Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 52 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 428 2017-06-21

Name

Maria Ndilla Kangoye

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIA N. KANGOYE aliuliza:-
Serikali imeziagiza Halmashauri zote za Wilaya nchini kutenga asilimia 10 ya mapato yake kwa ajili ya vijana na wanawake:-
Je, Serikali imetoa kiasi gani kwa vikundi vya vijana na wanawake tangu zoezi hilo lianze?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Maria Ndila Kangoye, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuanzia mwaka 2010 – 2016 Serikali imefanikiwa kutoa shilingi bilioni 122.4 kwa ajili ya mikopo ya vijana na wanawake ambazo zinatokana na asilimia kumi iliyotengwa kila mwaka kutokana na mapato ya ndani ya Halmashauri. Katika mwaka wa fedha 2016/2017, Serikali imepanga kutoa shilingi bilioni 56.8 ambapo mpaka mwezi Machi 2017 zimeshapelekwa shilingi bilioni 17.3 kwenye vikundi vya wanawake na vijana. Serikali itaendelea kutenga fedha hizo kila mwaka ambapo katika mwaka wa fedha 2017/2018, Serikali imeshatenga shilingi bilioni 61.