Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 54 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 444 2017-06-23

Name

Gibson Blasius Meiseyeki

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. GIBSON B. OLE MEISEYEKI aliuliza:-
Hivi karibuni Serikali ilianza zoezi la kubomoa nyumba kwenye vyanzo vya maji na waathirika wa operesheni hiyo sheria imewakuta na wengi wao walikuwa kwenye maeneo hayo tangu enzi za ukoloni hususani wananchi wa Kata ya Kiranyi:-
Je, Serikali inawafikiriaje wananchi hawa ambao sheria imewakuta kwenye maeneo hayo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Gibson Blasius Ole-Meiseyeki, Mbunge wa Arumeru Magharibi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wa Kata ya Kiranyi na Olorien hutegemea kupata maji katika chanzo cha Sailoja katika Halamshauri ya Wilaya ya Arusha. Chanzo hiki kinahudumia sehemu ya Mamlaka ya Mji mdogo wa Ngaramtoni kwa ajili ya matumizi ya maji ya wakazi wa Mji huo na viunga vyake katika Jimbo la Arumeru Magharibi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Arusha imefanya utambuzi wa nyumba na mali zilizopo ndani ya chanzo cha maji cha Sailoja katika Kata ya Karanyi. Halmashauri inakusudia kukaa na watu ambao wamo ndani ya chanzo. Aidha, utambuzi wa awali umebainisha jumla ya Kaya 120 zimetambuliwa kwenye eneo la chanzo hicho cha maji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa Halmashauri ina mpango wa kukutana na wananchi ambao wamebainika kuwa katika chanzo hicho cha maji ili kufanya mazungumzo ya pamoja ya namna ambavyo utaratibu utakavyokuwa kwa kuzingatia sheria na miongozo iliyopo. Ofisi yangu itasimamia zoezi hili ili kuhakikisha kwamba sheria, kanuni na taratibu zinazingatiwa wakati wa kunusuru chanzo hiki.