Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 55 Energy and Minerals Wizara ya Madini 455 2017-06-28

Name

Dr. Pudenciana Wilfred Kikwembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Primary Question

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE aliuliza:-
Hitaji la kuni limekuwa kubwa kwa matumizi kama nishati ya kupikia na hivyo kusababisha uharibifu mkubwa wa mazingira:-
Je, Serikali itawezesha vipi wananchi kupata nishati mbadala kwa matumizi ya kupikia majumbani?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI (K.n.y. WAZIRI WA NISHATI NA MADINI) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Pudenciana Kikwembe, Mbunge wa Jimbo la Kavuu, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kwa kushirikiana na Kituo cha Uendelezaji na Usambazaji wa Teknolojia za Kilimo Vijijini (CAMARTEC) inaendelea na ujenzi wa mitambo ya bayogesi nchini kwa ajili ya kupikia na matumizi mengine majumbani, taasisi za Serikali zikiwemo shule, hospitali na Magereza. Hadi sasa mitambo ya bayogesi iliyojengwa inafikia 20,000. Lengo la kituo ni kujenga jumla ya mitambo 22,000 kwa nchi nzima ifikapo mwaka 2018.
Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2009 Serikali kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC) ilianza kutekeleza mradi wa kusambaza gesi asilia katika baadhi ya maeneo ya Dar es Salaam kupitia mradi wa mfano (Pilot Project) kwa ajili ya kupikia majumbani. Hadi sasa hoteli tatu, gereza moja, nyumba 70 na viwanda 36 vinatumia gesi asilia.
Mheshimiwa Naibu Spika, TPDC imekamilisha upembuzi yakinifu kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya usambazaji wa Gesi Asilia katika Mikoa ya Dar es Salaam, Lindi na Mtwara. Miradi ya usambazaji wa gesi asili katika mikoa hiyo utaanza mwaka 2018 na kukamilika mwaka wa 2020/2021 kwa kuwafikishia gesi wateja wapatao 50,410. Miradi hii itagharimu jumla ya dola za Marekani milioni 126.959.
Mheshimiwa Naibu Spika, mwezi Julai, 2017, Serikali kupitia TPDC itaanza kutekeleza mpango wa kupeleka gesi majumbani katika mikoa mingine ya Tanzania Bara ili kuhakikisha wananchi wote wanafikiwa na huduma hii.