Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 56 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 462 2017-06-29

Name

Njalu Daudi Silanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Itilima

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO (k.n.y MHE. NJALU D. SILANGA) aliuliza:-
Wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu mwaka 2015, Mheshimiwa Rais aliahidi kujenga nyumba za watumishi katika Makao Makuu ya Wilaya ya Itilima katika Kijiji cha Langabidili. Je, ni lini ahadi hiyo itaanza kutekelezwa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NABU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Njalu Daudi Silanga, Mbunge wa Itilima kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Itilima ni kati ya Wilaya tano zinazounda Mkoa wa Simiyu. Wilaya hii ilianzishwa mwaka 2012 kwa GN Na. 73, na Halmashauri yake ilianzishwa mwezi Mei, 2013 kwa GN Na. 47. Wilaya ya Itilima imezaliwa kutoka katika Wilaya ya Bariadi na kuunda Mkoa wa Simiyu wenye Wilaya tano na Halmashauri sita. Watumishi wa Halmashauri wanalazika kuishi Bariadi Mjini na kusafiri umbali wa kilometa 33 kila siku kutoka Bariadi hadi Makao Makuu ya Wilaya kwa ajili ya kufanya kazi.
Mheshimiwa Spika, kutokana na usumbufu na gharama za usafiri Serikali ilitoa shilingi milioni 500 kwa mwaka wa fedha 2014/2015 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za watumishi na kulipa fidia maeneo ya wananchi. Hadi sasa ujenzi wa nyumba nne unaendelea katika hatua za mwisho.
Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha 2016/2017 Serikali ilitenga shilingi milioni 230 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba nne za wananchi. Aidha, Serikali imetoa shilingi milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji. Ujenzi unaendelea na unatekelezwa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA).
Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2017/ 2018, Serikali imetenga shilingi milioni 250 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba nyingine nne za watumishi. Serikali itaendelea kutenga fedha kidogo kidogo kwa kadri zitakavyopatikana ili kuweza kukamilisha nyumba za watumishi.