Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 56 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 467 2017-06-29

Name

Taska Restituta Mbogo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza:-
Mkoa wa Katavi hauna umeme wa Gridi ya Taifa. Je, ni lini Mkoa huo utapatiwa umeme wa Gridi ya Taifa?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI (K.n.y. WAZIRI WA NISHATI NA MADINI) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Taska Restituta Mbogo, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Katavi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa Mikoa ya Kusini Magharibi ikiwemo Katavi, Kigoma na Rukwa kuunganishwa na umeme wa Gridi ya Taifa. Serikali kupitia TANESCO imeanza utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme wa Gridi Msongo wa kilowati 400 yenye urefu wa kilometa 1,080 kutoka Mbeya – Sumbawanga – Mpanda – Kigoma hadi Nyakanazi.
Mheshimiwa Spika, mtaalam mshauri amekamilisha kazi ya kudurusu taarifa ya upembuzi yakinifu kwa ajili ya kuhuisha mradi kutoka kilovoti 220 hadi kilovoti 400. Utekelezaji wa ujenzi wa mradi huu utaanza mwezi Desemba, 2017 na kukamilika mwaka wa fedha 2018/2019 ambapo Mkoa wa Katavi utaanza kupata umeme wa Gridi ya Taifa. Gharama za mradi ni dola za Marekani milioni 664.