Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 57 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 476 2017-06-30

Name

Frank George Mwakajoka

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA aliuliza:-
Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusiana na ada ya Zimamoto ambayo wanatozwa wafanyabiashara katika Halmashauri ya Mji wa Tunduru huku kukiwa hakuna Jeshi la Zimamoto na Uokoaji eneo hilo?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Frank Mwakajoka, Mbunge wa Tunduma kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ada zinazotozwa na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji ni kwa mujibu wa Sheria Na. 14 ya 2007 ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na Kanuni za Ukaguzi za mwaka 2008 na Marekebisho yake ya mwaka 2012 na 2014. Sheria na Kanuni hizi zinamtaka mmiliki wa chombo cha usafiri pamoja na usafirishaji, mmiliki wa jengo refu au fupi, chombo cha usafiri na usafirishaji, mfanyabiashara au ofisi kulipia tozo ya ukaguzi. Tozo hizo zimepangwa kutokana na ukubwa wa jengo na hatari ya moto kwenye eneo husika.
Mheshimiwa Spika, katika Wilaya ya Momba Mkoani Songwe, Halmashauri ya Tunduma ina kituo cha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji ambacho kipo katika Mtaa wa Kilimanjaro na kina askari kumi na gari moja la kuzimia moto. Kwa sasa gari hilo lipo Jijini Mbeya kwa ajili ya matengenezo. Wizara kupitia Jeshi la Zimamoto na Uokoaji inafanya jitihada za haraka ili gari hilo litengamae na kurejea kituoni.
Mheshimiwa Spika, hata hivyo, askari wa Jeshi la Zimamoto na uokoaji wanaendelea na majukumu yao mengine ya kutoa elimu ya kinga na tahadhari za moto na ukaguzi wa majengo ili kuzuia ajali za moto na majanga mengine. (Makofi)